Akaunti ya Akiba ya ELIMU inamuwezesha mwanachama kuchangia kwa hiari yake mwenyewe ili kukidhi mahitaji ya kulipa karo za shule/chuo kwa ajili yake, ndugu au wategemezi wake.


FAIDA ZA AKAUNTI YA AKIBA YA ELIMU

  1. Akiba itazaa faida ya Riba Juu ya Akiba (Interest on Savings) kila Mwaka
  2. Akiba ya Elimu inakuwezesha kupata Mkopo wa Elimu ambao ni mara mbili (2) ya Akiba ya Elimu 
  3. Unaweza kupunguza Akiba ya Elimu mara nne(4) kwa mwaka (Kila robo mwaka mara moja) ikiwa fedha inayopunguzwa haiathiri dhamana ya Mkopo wa Elimu.
  4. Malipo hufanyika ndani ya masaa 24 endapo mwanachama akitaka kupunguza kiasi cha Akiba ya Elimu kwa njia ya Simu au Benki.
  5.  Mwanachama anaweza kuchangia katika Akaunti hii kila anapopata fedha (Kwa njia ya Mshahara au Kuweka fedha katika akaunti za chama au Makubaliano ya Bank Standing Order).

 

VIGEZO NA MASHARTI

  1. Kiwango cha chini cha kuweka ni TZS. 50,000

 

AKAUNTI ZA BENKI ZA CHAMA

Jina la Akaunti ni: TRA SACCOS LTD:

  • NBC 012103020266,
  • CRDB 01J1328947802,
  • NMB 20310008081,
  • AZANIA 00100021049

 

JINSI YA KUFUNGUA AKAUNTI YA AKIBA YA ELIMU

  1. Bofya hapa, jaza fomu itakayotokea, pakua .PDF dokumenti, kisha itume kwenye barua pepe ya Chama (This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.)