TRA SACCOS
  • Home
  • About Us
  • Products
  • Forms
  • Members Portal
  • FAQ
  • Contact us

Kuhusu TRA SACCOS

  • Dira, Dhima, na Malengo
  • Utawala
  • Muundo wa Chama
  • Bodi
  • Sheria na Kanuni

Mikopo

  • Maendeleo ya Jamii
  • Dharura
  • Papo kwa Papo
  • Week End
  • Mkopo wa Elimu
  • Mkopo wa Jipange

Akaunti za Akiba

  • Akaunti ya WEKEZA
  • Akaunti ya Akiba ya Elimu
  • Akaunti ya Akiba ya Afya
  • Akaunti ya Maandalizi ya Kustaafu
  • Huduma ya Rambirambi
  • Akaunti ya Akiba ya Lazima

Uncategorised

Welcome to TRA SACCOS LTD Website

TRA SACCOS LTD is a registered Savings and Credit Co-operative Society whose main objective is to mobilize savings from members and in return provide credit facilities. TRA SACCOS LTD is an employee-based SACCOS which was established under the current governing Co-operative Societies ACT No 20 of 2003 in 2006 and Licensed as Class B under microfinance act No 10 of 2018 in 2021. Other objectives of the SACCOS are to encourage thrift among its members by educating the members the advantages of developing a savings behavior, through proper investment best practices aimed at improving the social and economic conditions of the members. This is achieved by offering the members complementary savings schemes, credit facilities and other financial products as may be required by the members from time to time.

 

AKAUNTI ZA BENKI ZA CHAMA

Jina la Akaunti ni: TRA SACCOS LTD:

  • NBC 012103020266,
  • CRDB 01J1328947802,
  • NMB 20310008081,
  • AZANIA 001000210497

Weekend Loan

1.0 Mkopo wa Weekend (Mkopo wa Sekunde)

Mkopo wa Weekend ni mkopo  unaopatikana mtandaoni muda wote (24/7) kwa wanachama wa TRA SACCOS. Mkopo huu umebuniwa ili kukupa fedha kwa haraka pale unapohitaji ili kutatua changamoto/mahitaji ya haraka.

Sifa za Mkopo wa Weekend

  • Mwanachama hupata mkopo ndani ya sekunde chache baada ya kufanya maombi

  • Kiwango cha juu cha mkopo: TZS 200,000.00

  • Riba ya mkopo ni 5%

    • Mfano: Ukikopa TZS 200,000, utalipa TZS 210,000

  • Muda wa marejesho ni hadi siku 30 tangu tarehe ya mkopo

  • Mkopo huu hauhitaji dhamana

  • Adhabu ya kuchelewesha malipo ni 5% kwa kila mwezi

  • Mkopo unapatikana kupitia:

    • Mobile Application – TRA SACCOS Kiganjani

    • USSD – *150*45#

    • Members Portal- (Internet Banking)

Pakua TRA SACCOS Kiganjani 

Inapatikana kwenye:
                           Get it on Google Play

                         


1.2 Vigezo na Masharti

  • Mwanachama atakayepitiliza muda wa marejesho (siku 30) atalipa adhabu ya 5% na kufungiwa kutumia huduma hii kwa miezi mitatu (3)

  • Mwanachama hataruhusiwa kupata mkopo mpya endapo:

    • Ana deni la Mkopo wa Weekend 

    • Amechelewesha marejesho au ku-default mkopo mwingine

    • Ana hisa chini ya TZS 1,000,000

  • Mabadiliko yoyote ya namba ya simu uliyowasilisha kwa SACCOS yaripotiwe mara moja ili kuepuka uvujaji wa taarifa zako za kifedha


1.3 Kujiunga na Huduma za Mtandaoni

Ili kuomba Mkopo wa Weekend, mwanachama anatakiwa kujiunga na huduma za mtandaoni kwa kufuata utaratibu ufuatao:

  1. Kujaza Fomu ya Kufungua Akaunti ya JIKIMU kwa ajili ya Kuunganishwa na Huduma za USSD (*150*45#) / TRA SACCOS Kiganjani

  2. Kwa Internet Banking, mwanachama atahuisha taarifa zake kupitia fomu ya huduma za mtandaoni inayopatikana kwenye tovuti ya TRA SACCOS

  3. Fomu ijazwe na kutumwa kupitia barua pepe: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

  4. Maombi yatafanyiwa kazi ndani ya masaa 12, na mwanachama atapokea taarifa za siri (credentials) kupitia SMS

  5. Mwanachama anatakiwa kubadilisha PIN kupitia:

    • USSD: *150*45#

    • Au kwa kusajili akaunti kwenye TRA SACCOS Kiganjani


2.0 Jinsi ya Kupata Mkopo

Baada ya kupokea taarifa za siri (credentials), mwanachama anaweza kuomba mkopo huu wakati wowote.


2.1 Kupitia Mobile App – TRA SACCOS Kiganjani

  1. Ingia (Login) kwenye TRA SACCOS Kiganjani

  2. Nenda kwenye Menu → Apply Application

  3. Chagua Loan Type: WEEKEND

  4. Weka kiasi unachohitaji

  5. Bonyeza REQUEST LOAN

 Muamala utafanyika papo hapo na fedha itaingia kwenye JIKIMU Akaunti yako

Matumizi ya Fedha

Baada ya fedha kuingia JIKIMU Akaunti, unaweza:

  • Kutoa kupitia M-Pesa, Airtel Money, Tigo Pesa, Ezy Pesa, T-Pesa, HaloPesa

  • Kutoa kupitia ATM za Umoja Switch (Cardless Withdrawal)

  • Kulipia huduma ndani ya Chama:

    • Hisa

    • Mikopo mingine

  • Malipo ya Bill Mbalimbali kama Maji, Umeme, SGR, TV n.k

2.2 Kupitia USSD

  1. Piga *150*45#

  2. Kama ni mara ya kwanza:

    • Tengeneza PIN ya tarakimu 4 baada ya kupokea credentials

  3. Ingia kwenye mfumo kwa PIN yako

  4. Chagua Weekend Loan

  5. Idhinisha maombi

 Fedha itaingia mara moja kwenye JIKIMU Akaunti yako na unaweza kuitumia kama ilivyoelekezwa hapo juu.


3.0 Jinsi ya Kulipa Mkopo wa Weekend

Malipo hufanyika kupitia JIKIMU Akaunti yako.

Hatua za Kulipa

  1. Tuma fedha kwenda JIKIMU Akaunti yako kutoka:

    • Mitandao ya simu (MNOs)

    • Benki

  2. Ingia kupitia:

    • USSD: *150*45#

    • Au TRA SACCOS Kiganjani

  3. Chagua TRANSFER → WEEKEND LOAN ACCOUNT

  4. Weka kiasi cha deni kinachodaiwa

Mfano:
Ulikopa TZS 200,000, utalipa TZS 210,000

Baada ya malipo:

  • Salio la WEEKEND LOAN Account litasoma 0.00

  • Akaunti ya mkopo itafungwa moja kwa moja

Endapo kutakuwa na changamoto yoyote, wasiliana na watendaji wa TRA SACCOS kwa msaada zaidi.


AKAUNTI ZA BENKI ZA CHAMA

Jina la Akaunti: TRA SACCOS LTD

  • NBC: 012103020266

  • CRDB: 01J1328947802

  • NMB: 20310008081

  • AZANIA: 00100021049

Mkopo wa Sikukuu

MKOPO WA SIKUKUU (SIKUKUU LOAN)

1.0 Utangulizi

Mkopo wa Sikukuu ni huduma maalum ya kifedha inayotolewa na TRA SACCOS LTD kwa wanachama wake wakati wa msimu wa sikukuu. Mkopo huu unapatikana kwa njia ya mtandao ndani ya siku saba kabla ya sikukuu husika, kwa lengo la kuwasaidia wanachama kukidhi mahitaji yao muhimu kipindi cha sikukuu.


1.1 Sifa za Mkopo wa Sikukuu

Mkopo wa Sikukuu una sifa zifuatazo:

  • Hutolewa wakati wa sikukuu pekee kama vile Krismasi, Pasaka, Idd, Mwaka Mpya na sikukuu nyingine rasmi

  • Hautegemei akiba wala hauna dhamana

  • Unapatikana kupitia njia zifuatazo:

    • Mobile Application ya TRA SACCOS Kiganjani

    • USSD *150*45#

    • Internet Banking (Self Service)

  • Unawahusu wanachama waliokamilisha Fomu ya Kufungua Akaunti ya JIKIMU

  • Kiwango cha juu cha mkopo ni TZS 500,000

  • Muda wa marejesho ni miezi 3

  • Riba ni 3% (Reducing Balance)

  • Mwanachama aliye kwenye orodha ya wadaiwa (Defaulter) hatastahili mkopo huu

  • Mwanachama anatakiwa kuhakikisha taarifa zake za mawasiliano, hususan namba ya simu, ziko sahihi na zinaripotiwa mapema endapo zitabadilika, kwa ajili ya usalama wa taarifa zake za kifedha


1.2 Vigezo na Masharti

Masharti ya Mkopo wa Sikukuu ni kama ifuatavyo:

  • Mwanachama atakayeshindwa kulipa mkopo ndani ya muda wa miezi 3:

    • Atatozwa adhabu ya 5%

    • Atazuiwa kutumia huduma ya Mkopo wa Sikukuu kwa kipindi cha miezi mitatu

  • Mwanachama hataruhusiwa kupata mkopo mpya endapo:

    • Bado ana deni la Mkopo wa Sikukuu

    • Ame-default mkopo mwingine wowote ndani ya chama

    • Ana hisa pungufu ya TZS 1,000,000

  • Mabadiliko yoyote ya namba ya simu iliyowasilishwa kwa SACCOS yaripotiwe mara moja ili kuepuka uvujaji wa taarifa za kifedha


1.3 Kujiunga na Huduma za Mtandaoni

Ili mwanachama aweze kuomba Mkopo wa Sikukuu, anatakiwa kujiunga na huduma za mtandaoni kwa kufuata hatua zifuatazo:

  1. Kujaza Fomu ya Kufungua Akaunti ya JIKIMU, inayopatikana kwenye tovuti ya TRA SACCOS

  2. Kutuma fomu hiyo iliyojazwa kwenda barua pepe: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

  3. Maombi yatafanyiwa kazi ndani ya masaa 12

  4. Mwanachama atapokea taarifa za siri za kuanzia (Credentials) kupitia ujumbe mfupi wa simu (SMS)

  5. Mwanachama atatakiwa kubadilisha PIN mara moja kupitia:

    • USSD *150*45#, au

    • Mobile Application ya TRA SACCOS Kiganjani


2.0 Jinsi ya Kuomba Mkopo wa Sikukuu

Baada ya kupokea taarifa za siri, mwanachama anaweza kuomba Mkopo wa Sikukuu muda wowote wakati wa dirisha la sikukuu lililotangazwa.


2.1 Kuomba Mkopo Kupitia Mobile Application

Mwanachama atatakiwa kufuata hatua zifuatazo:

  1. Kuingia (Login) kwenye TRA SACCOS Kiganjani baada ya kubadilisha PIN

  2. Kuchagua Menu → Apply Application

  3. Kuchagua Loan Type: SIKUKUU

  4. Kuingiza kiasi cha mkopo kinachohitajika

  5. Kubofya REQUEST LOAN

Baada ya ombi kufanyiwa kazi, fedha itawekwa kwenye JIKIMU Akaunti ya mwanachama.

Fedha hiyo inaweza kutumika kwa:

  • Kutoa kupitia mitandao ya simu (M-Pesa, Airtel Money, Tigo Pesa, Ezy Pesa, T-Pesa, Halo-Pesa)

  • Kutoa kupitia ATM za Umoja Switch (Cardless Withdrawal)

  • Kulipia hisa, mikopo mingine, au malipo ya huduma mbalimbali kama maji, umeme, SGR, TV na huduma nyingine ndani ya chama

Pakua TRA SACCOS Kiganjani   Get it on Google Play

                                                 


2.2 Kuomba Mkopo Kupitia USSD

Hatua za kuomba mkopo kwa njia ya USSD ni kama ifuatavyo:

  1. Piga *150*45#

  2. Endapo ni matumizi ya mara ya kwanza, tengeneza PIN ya tarakimu 4 baada ya kupokea credentials

  3. Ingia tena kwa kupiga *150*45#

  4. Fuata maelekezo kwenye simu

  5. Chagua Sikukuu Loan

  6. Thibitisha ombi

Fedha itaingia moja kwa moja kwenye JIKIMU Akaunti ya mwanachama.


3.0 Jinsi ya Kulipa Mkopo wa Sikukuu

Malipo ya Mkopo wa Sikukuu hufanyika kupitia JIKIMU Akaunti ya mwanachama kwa utaratibu ufuatao:

  1. Ingiza fedha kwenye JIKIMU Akaunti kupitia mitandao ya simu au benki

  2. Ingia kwenye:

    • USSD *150*45#, au

    • Mobile Application ya TRA SACCOS Kiganjani

  3. Chagua TRANSFER

  4. Hamisha fedha kwenda SIKUKUU LOAN ACCOUNT

  5. Weka kiasi cha deni kinachodaiwa

  6. Thibitisha muamala kwa kubonyeza SEND MONEY

Baada ya mkopo kulipwa kikamilifu:

  • Salio la Akaunti ya Mkopo wa Sikukuu litasoma 0.00

  • Akaunti ya mkopo itafungwa rasmi

Endapo kutatokea changamoto yoyote, mwanachama anashauriwa kuwasiliana na watendaji wa TRA SACCOS kwa msaada zaidi.


4.0 Akaunti za Benki za Chama

Jina la Akaunti: TRA SACCOS LTD

  • NBC: 012103020266

  • CRDB: 01J1328947802

  • NMB: 20310008081

  • AZANIA BANK: 00100021049

Mkutano Wa Wanachama kwa Vituo vya Dar es Salaam 2025

TRA SACCOS LTD INAWAKARIBISHA WANACHAMA WOTE WA VITUO VYA DAR ES SALAAM KWENYE MKUTANO WA MAANDALIZI YA AGM 2025:

Ndugu Mwanachama,

Kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu, Mkutano wa Vituo vya DSM uliopaswa kufanyika wikiendi iliyopita ya tarehe 1 & 2 Novemba, sasa utafanyika siku ya Jumamosi na Jumapili, tarehe 8 na 9 Novemba 2025.

Mahali: Katika Ukumbi wa Multipurpose  Hall - Chuo cha Kodi (ITA) -Mikocheni Industraial Area

Muda:Kuanzia saa 1:30 asubuhi, kwa kuzingatia mgawanyo wa vituo wa awali.

RATIBA YA VITUO:

Wataohudhuria Tarehe 8: Wataohudhuria Tarehe 9:

LTD HQ,ICDS,KINONDONI,ILALA I,ILALA II,KARIAKOO,HQ-I,HQ-II ,TEMEKE,DRD HQ,ICT

WHARF ,CSC ,FAST TMU, HQ-III ,HQ-IV, JNIA, PCA, SCANNER, TEGETA, CSC-HQ, ITA, MTD HQ, CSC-MAFUTA, BUGURUNI, OUT OF TRA, RETIRED TRA, TRA IN KENYA and TRANSFERRED MANZESE UPANGA KIMARA

CHA KUZINGATIA:

Tafadhali hakikisha unahudhuria, kwani huu ni Mkutano muhimu kwa maendeleo ya Chama Chetu. Usisahau kitambulisho cha kazi kwa ajili ya usajili.

Ratiba:

MUDA

DAKIKA

TUKIO/MADA

MHUSIKA

01:30 – 03:00 Asubuhi

90

KUJIANDIKISHA NA KUINGIA UKUMBINI

WOTE

03:00 – 03:10 Asubuhi

10

SALA/DUA

MJUMBE ALIYECHAGULIWA

03:10 – 03:30 Asubuhi

20

UTAMBULISHO NA SALAMU ZA UKARIBISHO.

MWENYEKITI

03:30 - 4:30 Asubuhi

60

UWASILISHAJI WA BAJETI YA MWAKA 2026

MENEJA

04:30 - 5:00 Asubuhi

30

UWASILISHAJI WA MAPENDEKEZO YA BIDHAA NA KUFUNGUA FUNGAMANO

MENEJA

05:00 - 05:45 Asubuhi

45

MAPUMZIKO YA CHAI

WOTE

05:45 Asubuhi – 06:20 Mchana

35

MJADALA

WOTE

06:20 – 06:30 Mchana

 

SALA/DUA

MJUMBE ALIYECHAGULIWA

Karibu sana!

 

Page 1 of 2

  • 1
  • 2
  1. You are here:  
  2. Home
  3. Uncategorised

Products

wastaafuaccount.gif

News

Kupanda kiwango cha HISA hadi TZS 1,000,000

Njia rasmi za mawasiliano

Akaunti Ya Wekeza

  Bofya Hapa Kuomba Mkopo wa Week-end

Jinsi ya Kulipa Mkopo wa Week-end